Kamati ya Bajeti Kufanya Mkutano wa Wadau wote wa masuala ya kodi


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kwa mujibu wa Kanuni ya 118 ya Kanuni za Kudumu za Bunge, Toleo la mwaka 2016, Nyongeza ya Nane, Sehemu ya Tatu Kifungu cha 9, imepewa jukumu la kusikiliza maoni na mapendekezo ya wadau kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha kila mwaka.


Katika kutekeleza jukumu hilo, Kamati ya Bajeti imepanga kufanya Mkutano wa Wadau wote wa masuala ya kodi (Public Hearing) kwa ajili ya kusikiliza maoni yao na mapendekezo kuhusu Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2016.


Mkutano huo umepangwa kufanyika siku ya Alhamisi Tarehe 16 Juni 2016 kuanzia Saa Tano asubuhi katika Ukumbi wa Pius Msekwa, Mkoani Dodoma.

Kwa kuzingatia umuhimu wa Muswada huo, Kamati inawaalika wadau wote kufika na kuwasilisha maoni yao kabla haujapelekwa katika hatua nyingine.


Maoni ya wadau yanaweza pia kuwasilishwa kwa njia ya Posta au Barua pepe kwa anuani ifuatayo:


Katibu wa Bunge,
Ofisi ya Bunge,
S.L.P 941,
DODOMA
Barua pepe: cna@bunge.go.tz

Imetolewa na,
Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano. Ofisi
Newer Posts Older Posts
© Copyright UCHAMBUZI LEO | Modified By Smart WEB
Back To Top Back To Top